Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya, leo imepokea msaada wa mifuko 150 ya saruji kutoka kwa wanachama wa New MZRH SACCOS ikiwa ni sehemu ya kurudisha kwa jamii kwa mwaka huu, msaada unaolenga kusaidia ujenzi wa vyumba vya upasuaji unaoendelea kwaajili ya kuboresha huduma za afya kwa wananchi.


Vilevile Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi Dkt. Dino Mwaja amewashukuru Wananchama wao kwa moyo wao wa kujitolea na kueleza kuwa msaada huo umekuja kwa wakati muafaka ili kuwezesha kazi ya ujenzi kuendelea na kueleza kuwa msaada huo wa saruji ni hatua muhimu katika kuhakikisha hospitali inakamilisha ujenzi wa vyumba vya theater, ambayo ni sehemu muhimu katika kutoa huduma bora za afya kwa wagojwa. Wananchi wa Mbeya sasa wanatarajia huduma bora zaidi za afya kupitia miradi hii inayoendelea.