SW | EN
SW | EN
URT Logo
The United Republic of Tanzania
Ministry of Health
Mbeya Zonal Referral Hospital
MZRH Logo

WATARAJALI WATOA ZAWADI WODI YA WATOTO WACHANGA HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA

Ikiwa ni tarehe 14 oktoba. 2024 siku ya kumbukizi ya miaka 25 ya kifo cha Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambara Nyerere watarajali kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya wametumia siku hii kwa kutembelea na kutoa zawadi mbalimbali wodi ya watoto Wachanga katika kitengo cha wazazi Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya.

Akiongea baada ya kukabidhi zawadi Kiongozi wa Watarajali Hospitalini hapa Dkt. George Andrew amesema wameona katika siku hii ya leo watumie nafasi ya kumuenzi baba wa taifa kwa kutembelea na kutoa zawadi hizo katika wodi hizo za watoto wachanga hospitalini hapa kwa lengo la kuwashika mkono na kuwatia moyo wagonjwa.

“…tumeona tutumie siku hii ya kumbukizi ya kifo cha Baba wa Taifa kuwatembelea wagonjwa na kuwatia moyo katika wodi hii ya watoto wachanga.” – Dkt. George Andrew
Kwa upande wake mkuu wa Kitengo hicho cha watoto wachanga Dkt. Rehema Marando amewashukuru kwa msaada huo na kuwataka waendelee kuwa na moyo huo wa kuwatembelea na kuwatia moyo wagonjwa hospitalini hapa.

“… nipende kushukuru kwa zawadi hizi na kuendelea kuwaomba muendelee na moyo huo wa kutoa hasa kwa wahitaji na wagonjwa hospitalini.” – Dkt. Rehema Marando

Zawadi zilizotolewa ni pamoja na katoni za Sabuni za unga, sabuni za kipande, mafuta ya kupaka watoto, pamoja na Pampasi.